Vijana kwa wakongwe wote walijitokeza kushiriki uchaguzi huo ambao wadadis wanasema umegeuka sarakasi
Uchaguzi wa Malawi umekumbwa na wimbi la mivutano miongoni mwa vyama vikuu vya siasa vilivyo simamisha wagombea urais wa nchi hiyo.
Dalili za kujitokeza kwa matatizo zilianza mapema siku mbili baada ya uchaguzi ambapo baadhi ya vyama kikiwemo chama tawala Peoples Party cha Rais Dr Joyce Banda walilalamika kuwa kuna mchezo mchafu umefanyika katika shughuli nzima ya upigaji kura.
Siku chache zilizopita Rais Banda alitoa amari ya kuufuta uchaguzi huo na kuitisha uchaguzi mwingine baada ya siku 90 kwa madai ya wizi na ulaghai uliokumba uchaguzi, lakini Mahakama kuu ilisema hana mamlaka hayo.
Siku mbili baadaye tume ya uchaguzi MEC chini ya mwenyekiti wake Jaji Mackson Mbendera, ikatangaza kuwa ni kweli imegundua ubadhirifu katika baadhi ya maeneo na hivyo lazima kura zote zihesabiwe upya.
Kufikia sasa haijajulikana nini itakuwa hatma ya kura zilizopigwa na wananchi zaidi milioni saba wa nchi hiyo huku vyama vya DPP na MCP kila kimoja kikidai kuwa kilielekea kushinda uchaguzi huo
Comments
Post a Comment